Saturday, August 16, 2008

Manispaa ya Morogoro yaboresha miundombinu

Manispaa ya mji wa Morogoro inaendelea kuboresha barabara zake kuu zinazounganisha mji huo. Barabara ambazo zinakaribia kukamilika kwa kiwango cha lami ni ile ya Uhuru inayopita benki ya "National Microfinance (NMB) na ile inayotoka njia panda ya Hospitali Kuu wa Mkoa hadi Morogoro Hotel na kupandisha hadi "uzunguni" maji yatiririka! Huenda haya yakawa ni moja ya matayarisho ya kuufanya mji huu kuwa JIJI. Barabara hizi na nyingine zikikamilika zitapinguza vumbi kwenye mji huo na kuboresha usafiri pia kuufanya upendeze. Morogoro ni moja kati ya miji maarufu na inayopendwa na watanzania na wageni kwa vile ina huduma muhimu na hali ya hewa ni nzuri.Tusubiri tuone.

No comments: