Friday, August 22, 2008

Habari ya bilioni 9 za wakulima kuwekwa kushoto uk 18 si sahihi

Leo nimepata fursa ya kulisoma gazeti la serikali la "Daily News" katika ukurasa wa 18 upande wa kushoto nakuta kichwa cha habari "Nanyumbu farmers Bask in rich harvest" kwa kuwa mimi ni mtu wa kilimo nashtushwa na habari hiyo. Nachimba zaidi napata habari kuwa wakulima wa karanga wa wilaya ya Nanyumbu wamepata zaidi ya shilingi bilioni 9 kwa kilimo cha karanga msimu huu wa 2007/08. Jamani bilioni 9 kwa kulima karanga kwa wilaya moja tena ya Tanzania hiyo siyo habari muhimu kweli? Kwa kweli mhariri hukuitendea haki habari hii. Mimi nilitazamia kuiona kwenye ukurasa wa kwanza tena upande wa kulia. Lakini hapa imewekwa ukurasa wa 18 kushoto!

No comments: