Friday, August 1, 2008

Viazi, mihogo hadi barabarani


Wakulima wetu wanajituma sana katika uzalishaji licha ya mazingira magumu waliyonayo lakini wameza kulisha taifa hili na kuweza kuimarisha uchumi wa nchi hii kupitia kilimo na ufugaji.


Juzi nilitembelea soko la Mbagala. Nilishangaa kuona mazao mbalimbali ya kilimo yamefurika soko hadi kuzagaa kwenye barabara.Muhogo na viazi bwerere kabisa. Ndani ya soko nyanya,bamia, mchele, maharage, vitunguu, karoti,mchicha, kabichi, mbaazi, njegere, ndimu, karanga, matango, pilipili hoho, pilipili mbuzi, tangawizi, nyanya chungu na vingine vingi vyote hivyo vimezalishwa na wakulima wadogowadogo. Licha ya kutegemea kilimo cha mvua kwa silimia kubwa lakini vyakula vipo. Kwa kweli wakulima wetu wanafanya kazi kubwa sana lakini bado mtazamo wa nchi kwenye kilimo naweza kusema ni hasi! Maneno mengi lakini wakulima tuseme ukweli hawajaendelezwa katika kilimo na hii inatokana na bajeti finyu inayotolewa kwa sekta ya kilimo

No comments: