Wednesday, August 6, 2008

Gwami Internet Cafe Morogoro

Mji wa Morogoro unapanda chati kwa kasi ya ajabu. Hii pengine inatokana na taasisi nyingi kuwepo kwenye mji huu. Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Chuo Kikuu Mzumbe, Chuo Kikuu cha Kiislamu, Chuo cha Ardhi, VETA Morogoro, Hospitali ya Mkoa, Chuo cha Mifugo, Stesheni ya Gari Moshi (Reli) Shule za Sekondari nyingi tu, kumbi za mikutano , mahoteli na nyumba za wageni na nyingine ambazo sijazitaja. Mji huu ni wa biashara hasa yanayotokana na mazao ya kilimo na madini.

Kuwepo kwa taasisi hizi kunasababisha kuongezeka kwa idadi ya wakazi na wageni wa mji huu kila siku. Kwa kuwa wageni na wakazi wanaongezeka basi mahitaji huongezeka.

Moja ya huduma muhimu katika enzi hizi za sayansi na teknolojia ni ile ya mtandao au "Internet". Internet inasaidia sana katika kurahisisha mawasiliano. Kwa mji kama huu wenye Maprofesa, wataalamu wazamivu na wazamili pamoja na wanafunzi wa ngazi zote huduma hii ni muhimu.

Ukiwa Moro usihangaike sana ulizia ilipo ofisi ya CCM wilaya ya Morogoro karibu kabisa na mahali pa starehe panapoitwa Chipukizi utakuta Internet Cafe moja bomba sana inaitwa Gwami Internet Cafe.

Internet Cafe hii ni moja ya internet ya kisasa hapa nchini naweza kusema bila ya kuuma meno. Computer zake ni safi na mtandao una speed kubwa. Usafi ndani ya cafe ni wa hali ya juu, vijana wachangamfu na wenye utaalamu wa mtandao wanatoa huduma safi. Hata maji ya kunywa yapo ndani ya cafe yanayopatikana kupitia mashine maalum. Dakika 30 ya kutumia mtandao ni shilingi 400/= tu.

No comments: