Tuesday, August 12, 2008

Morogoro Internet kama kazi

Sasa ni saa tatu na dakika sita (6) usiku nipo ndani ya jiji la Moro. Siyo siri mwanangu mi niko kwenye mtandao. Ndiyo maana nimeweza kupost habari kama mbili tatu hivi. Kwa kweli siyo siri, Moro kumekucha. Nasikia kuna maoni yanaendelea kutolewa na wakazi wa jiji hili kama Moro inastahili kuwa Jiji? Pamoja na ukweli kuwa mimi ni Banzi wa Moro mambo bado kidogo. Manispaa inatakiwa kuboresha miundo mbinu ya mji wa huu hasa barabara. Hata ile barabara ya kwenda Mji Mpya bado ni ya udongo. DDC ileile aliyopiga Marehemu Mbaraka Mwinshehe na Cubano Marimba na yalipo makao Makuu ya Lugaluga Agricultural and Marketing Cooperative Society. Hata, lazima tuwe wa kweli. Mambo mengi mazuri yapo Moro, lakini hili la barabara lazima liboreshwe na usafi uboreshwe. Vingenevyo kwa mtandao tu Moro ni kama kazi.

No comments: