Tuesday, August 5, 2008

"B One" Mtandao bora wa nyumba za wageni Morogoro

Ukiwa ni mara yako ya kwanza kutembelea mji wa Morogoro usipate shida ulizia "B one" kwa ajili ya huduma za malazi.

Wiki iliyopita nilikuwa Morogoro. Huwa nauona mtandao wa B one wa nyumba za wageni lakini niseme ukweli nilikuwa naogopa kuulizia nikidhani kuwa ni za gharama kubwa yaani si ya kiwango changu. Kumbe nilikuwa sina taarifa sahihi za kutosha. Nilipojaribu kuulizia nafasi ya malazi nilibahatika kupta kwenye moja ya nyumba hizo. Lazima ni kiri kwa mambo yafuatayo niliyoyaona kwenye nyumba hiyo.
  • Usafi wa hali ya juu
  • Kauli nzuri ya wahudumu
  • Unapata kifungua kinywaji kamili (+juice ya matunda ya Morogoro!)
  • Ulinzi wa uhakika
  • Utulivu masaa 24
  • Kila chumba kina TV
  • Gharama ya kuridhisha

Kilichobaki "B One" ni kujitangaza kwa njia zote ikiwezekana kukamata soko la nyumba za wageni Morogoro. Kula 5 mjasiriamali wa "B one."

Kwa mtandao kama huu, Moro sasa chati yake inapanda kwa kasi ya kutisha. Tembelea Moro na usikose kuulizia "B one" halafu toa maoni yako kupitia www.innobanzi.blogspot.com

No comments: