Friday, August 22, 2008

Taasisi ya Utafiti Kilimo chanzo cha bilioni 9 Nanyumbu

Teknolojia ya mbegu bora za karanga kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo -Naliendele, Mtwara zimewawezesha wakulima wa karanga kuvuna tani 12,241 za karanga na hivyo kujipatia jumla ya shilingi bilioni 19.18 msimu wa 2007/08. Akitoa taarifa hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Nanyumbu Bw. Farid Mhina amesema kuwa zaidi ya asilimia 90 ya wakulima wa karanga wilayani humo wanatumia mbegu bora.

Karanga ni moja ya zao la biashara linalokuja kwa kasi katika wilaya ya Nanyumbu, huku Korosho ikishika nafasi ya kwanza kwa kuwa chanzo cha kipato cha wananchi wa Nanyumbu. Hii ni kwa mujibu wa gazeti la Daily News la tarehe 22/08/2008.

No comments: