Thursday, August 14, 2008

PROKON kuzalisha mafuta kutoka mbono

Kampuni ya PROKON kutoka Mpanda inatarajia kuanza kuzalisha mafuta kutoka mmea wa mbono ifikapo mwaka 2010.

Hayo yalielezwa na wawakilishi wa Kampuni hiyo kwenye maonyesho ya nane nane 2008 yaliyofanyika kwenye Uwanja wa John Mwakangale jijini Mbeya.

Wakiwa na sampuli ya mafuta hayo, ambayo ni mbadala wa mafuta ya petroli kwa kuendesha mitambo na magari, wawakilishi hao walieleza kuwa kwa sasa kiwanda kimeshaaanza kujengwa mjini Mpanda. Kilo moja ya mbegu za mbono kwa sasa zinauzwa kwa bei ya shilingi 1,200/= huko Mpanda, lakini mara nyingi bei huwa ni makubaliano kati ya mkulima na mfanyabiashara.

No comments: