Wednesday, August 13, 2008

Manispaa ya Sumbawanga yazalisha tani 64,338 za mahindi

Mahindi ni zao maarufu linalolimwa kwenye Manispaa ya Sumbawanga. Katika msimu wa 2007/08 Manispaa hiyo imeweza kuzalisha tani 64,338 za mahindi.Kiasi hicho ni kikubwa ikilinganishwa na uzalishaji wa mazao mengine yanayolimwa katika Manispaa hiyo. Mazao hayo ni kama vile Maharage (tani 8,100) na viazi vitamu (tani 13,622). Wakizungumza na blog hii, wakulima walioshiriki kwenye maonyesho hayo kwenye banda la Halmashauri hiyo, walisema kuwa utaalamu wa kilimo bora na teknolojia za kisasa hupata kutoka kwa maafisa ugani na kituo cha Utafiti wa Kilimo Uyole. Sumbawanga huzalisha pia chakula cha asili kijulikanacho kwa jina la kikanda ambalo husaidia kwa wagonjwa wa vidonda vya tumbo pamoja kuwapa wagonjwa hamu ya chakula.

No comments: