Monday, March 31, 2014

Petty Mloka kanisani Matombo

Petty Mloka (kushoto) akifuatilia kwa makini ibada ya Misa takatifu  ya kumuombea baba yake Balozi Daniel Mloka miaka 20 tangu aiage dunia hii. Kumbukumbu ilifanyika tarehe 22/03/2014 kijijini Matombo, Morogoro kushoto ni mtoto wake Nia .

Ibada ya kumbukumbu ya Miaka 20 ya kifo cha Balozi Daniel Mloka

Cesar Mloka na watoto wake Jews na Jordan wakiwa ndani ya Kanisa Katoloki Parokia ya Matombo wakati wa Ibada ya Misa Takatifu ya kumbukumbu ya Baba yake Marehemu Balozi Daniel Narcis Mtonga Mloka iliyofanyika tarehe 22/03/2014 kijijini Matombo,Morogoro.

Kaburi la mjomba Dr. Gregory Paul Constance Mluge

Dr. Mluge alikuwa mwema na mpole. Profesa wa Tiba. Dr Mluge aliiacha Dunia hii akiwa anapendwa.TUTAKUPENDA daima (Tafsiri yangu) . Ni mmoja wa wasomi waliotukuka wazaliwa wa Matombo mkoani Morogoro. Alizaliwa tarehe 12 Machi 1937 na kufariki tarehe 9 Juni 2012. Amezikwa kwenye makaburi ya Kanisa lake Parokia ya Matombo alikobatizwa na kupata, komunio na Kipaimra. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. AMINA

Darini kwa waimbaji kanisani Matombo

Nilibahatika kusali njia ya msalaba  Ijumaa ya tarehe 21/04/2014 kanisani Matombo. Nilipogeuka nyuma na kutazama juu nikaona sehemu ya darini walipokuwa wakikaa waimbaji na kuimba Noel ! Noel !ajaye Mtu MUNGU!  au Mkristu Miye niko salama shetani wee usinijie......Hakika siku zinapita kwa kasi na mabadiliko ni mengi. Wakati huo kinanda kilikuwa kikiporomoshwa na Babu marehemu Mwl. Paul Lugonzo au Marehemu Mwl. Isdori Baggo.Mungu awalaze mahali pema peponi AMINA. Siku hizi waimbaji wanaimba wakiwa mbele kanisani na huku kinanda kikiwa chini!

Sehemu ya 'Kupolisi' kanisani Matombo

Nilipokuwa mdogo nilimsikia Babu yangu Mzee Mwl. Ephrem  Kobelo a.k.a Mzee  Vibaya akinieleza kuwa sehemu hiyo iliyotengwa kanisani ni kwa ajili ya 'kupolisi'. Mara nyingi nilimuona Padri akishamaliza kusoma Injili hupanda ndani ya chombo hicho na kuanza kuhubiri. Siku hizi mapdri hawakitumii tena. Akiwa ndani ya chombo hicho waumini waliweza kumuona barabara naye kuwaona waumini. Na ikumbukwe kuwa wakati huo kulikuwa hakuna vipaaza sauti. Pengine sasa hatuhitaji tena chombo hiki kwani tuna vipaaza sauti. Tutawaeleza wajukuu wetu kuwa hiyo ni sehemu ya kupolisi. Huenda Paroko wa Matombo wa sasa Fr. Kobelo atakitumia chombo hiki wakati wa sherehe ya Pasaka mwaka 2014!

Hivi tunataka kuwamaliza hawa?

Kwa uroho wetu wa kupata utajiri wa harakaharaka kuna watu tunaowaita majangili wana mkakati wa kumaliza tembo hawa kwa lengo la kupata meno yao na kuyauza. Tulinde raslimali za taifa wakiwemo tembo. Wakiisha hawatapatikana tena.

Sehemu ya kufanya kitubio kanisani Matombo

Ndani ya Kanisa Katoliki Parokia ya Matombo kuna chombo mahususi kilichotengenezwa kwa kutoa kitubio kwa waumini. Kitubio ni kitu cha siri kati yako na Padri. Padri anamwakilisha  mwenyezi Mungu. Wakati huu wa Kwaresima wangapi tumeshafanya kitubio? Je tumeshakuwa na nia makusudi ya kuwaomba tuliowakosea watusamehe? Tafakari.

Twiga akiwa mbugani Mikumi-Morogoro

Mnyama twiga mrefu mwenye ngozi ya kuvutia na mwendo wa madaha anapataikana nchini Tanzania, hasa katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, Morogoro, Tanzania

Simba

Huyu ndiye simba dume akiwa kwenye hifadhi ya Taifa-Mikumi, Morogoro, Tanzania

Pundamilia michirizi haifanani

Ukipata bahati ya kuwaona pundamilia wengi unaweza kudhani kuwa michirizi ya ngozi yao hufanana. La hasha, wataalamu wanasema kuwa michirizi ya punda milia ni tofauti kwa kila mmoja.

Mafunzo kazini

Wizara na Taasisi zake hapa nchini hutenga bajeti ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wake kwa lengo la kuleta tija katika utendaji kazi. Pichani wanafunzi na walimu wao kutoka Taasisi ya Taifa ya Tija (NIP) mara baada ya kuhitimu mafunzo  mwezi Machi 2014 kituo cha Tushikamane mjini Morogoro. Bi Halima Yusufu wa Idara ya Utafiti na Maendeleo kituo cha Utafiti wa Kilimo Tanga  (wa tatu kutoka kulia waliosimam a mstari wa mbele) ni mmoja wa wanufaika wa mafunzo kazini aliyegharamiwa na mradi wa EAAPP. HONGERA. 

Dadaz wa Magomeni bado wapo

Kikundi cha sanaa maarufu kama Dadaz bado wanaendelea na shughuli za burudani. Walianza wakiwa wadogo sana sasa wameanza kuwa mamaz. Pichani wanaonekana wakitoa burudani kwenye siku ya kubariki Kanisa la Magomeni jimbo Kuu la Dar Es Salaam. (Picha kwa hisani ya Silyvester Jakka)

Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo abariki Kanisa la Magomeni








Tarehe  01 Machi 2014 Kanisa Katoliki Parokia ya Magomeni (Mashahidi wa Uganda) Jimbo  Kuu la Dar Es Salaam lilibarikiwa na Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo Askofu wa Jimbo hilo. Kanisa hilo lilibarikiwa baada ya kufanyiwa ukarabati mzito na kupata sura mpya kama inavyoonekana pichani. Nani alijenga sasa KANISA kama siyo MIMI na WEWE. Amina.(Picha zote kwa hisani ya Slyvester Jakka)

Thursday, March 27, 2014

Je unaweza kumvika mwenzi wako pete ya harusi kama hii?

Kuna aina nyingi za alsmasi na kuna wenywe uwezo wa kuzinunua hii ni 'Morganite Diamond'

Zoezi la kutambua mchumba

Dada wa Bi Harusi mtarajiwa (Ruthgard Mapunda) akiletwa hadharani kutambuliwa na mchumba wake

Kabla ya kukamilisha kulipa mahali ni lazima wachumba kutambuana. Usije ukuuziwa mbuzi kwenye gunia. Ndivyo ilivyokuwa katika shrehe ya kulipa mahali wakati Richard na familia yake walipokuja kutoa mahali ya kutaka kumchumbia Bi Ruthgard Prosper Mapunda wa Yombo, Dar Es Salaam

Richard anamtambua mchumba wake Ruthgard Mapunda

Raha ilioje unapoletewa chaguo lako na kujihakikishia  na mchumba kuonyesha furaha, hali ya kukubaliwa. Hongera Richard na Ruthgard kwa kuanza mchakato wa ndoa.  Picha ndogo juu - Ruthgard Prosper Mapunda alipokuwa mdogo.

Raha ya kijana kuchumbia

Ndugu apande wa Mume (mchumba wa Ruth) wakiserebuka mara tu kijana wao alipomtambua mchumba wake

Mzee Prosper Mapunda

Mzee Prosper Mapunda akiwa katika pilika za madalizi ya kupokea posa ya binti yake Ruthgard Prosper Mapunda shughuli iliyofanyika nyumbani kwake Yombo tarehe 23/3/2014 Jumapili. Mama Banzi na shem Mama Happy  (aliyebeba mtoto) walikuwepo kushuhudia tendo hilo. Banzi wa Moro alikuwa upande wa Mzee Mapunda.

Tuesday, March 25, 2014

Kumbukumbu ya Miaka 20 ya Marehemu Balozi Daniel Narcis Mtonga Mloka



Kaburi  alimozikwa Marehemu Balozi Daniel Mloka. Mwaka huu ni miaka 20 tangu afariki na kuzikwa kijijini kwao Matombo, Morogoro. Balozi Mloka atakumbukwa kwa kuchapa kazi, ukweli na ucheshi wake. Alisimamia aliyoyaamini bila kuyumba. Mwandishi aliyeondoka na kalamu yake na kuacha vitabu vingi vya falsafa nzito kama vile 'Baharia bila Meli.'

Kaburi la Mama Mzazi-Maria Patrick Mchiro

Hapa ndipo alipozikwa  Marehemu mama yangu  Maria Patrick Mchiro a.k.a Binti Jamunda takribani miaka 19 iliyopita. Alizaliwa mwaka 1937 na kufariki mwaka 1995  akiwa na umri wa miaka 58. MUNGU  mrehemu Mama yetu. AMINA

Sanamu ya Mt. Paulo kanisani Matombo

Kwa walio bahatika kusali ndani ya kanisa Katoliki Parokia ya Matombo wanaikumbuka sanamu hii ya Mt. Paulo somo wa Kanisa. Enzi zetu siku ya Sikukuu ya Petri na Paul ilikuwa ni maarufu Matombo. Siku hizi waumini hawajali kabisa sikukuu hii. Tukumbuke tulikotoka pengine kuna la kujifunza.

Usafiri- Morogoro-Matombo

Kutokana na kuimarishwa barabara ya Morogoro Matombo. Mabus  mengi husafiri kutoka Morogoro kwenda Matombo kila siku ni safari ya saa moja tu. Hivyo bus linaweza kufanya safari ya kwenda na kurudi kwa siku moja. Pichani ni bus la kutoka Morogoro kwenda Matombo-Tawa likishusha abiria kituoni Kiswira.

Monday, March 24, 2014

Matombo sekondari yapata umeme

Hakuna sababu tena ya wanafunzi kushindwa mitihani, hakuna sababu tena ya kukosa kutumia computer.Matombo Sekondari yapata umeme. Hongera sana

Matombo Secodnary School Netball ground

Uwanja wa mpira wa pete-Shule ya Sekondari Matombo

Kiwanja cha mpira Matombo Sekondari

Nimewahi kucheza mpira kwenye kiwanja hiki miaka ya sabini huku nikifunga magoli muhimu kwenye goli linaloonekana au wakati mwingine kufungwa na kuokoa michomo nikiwa golini. Kiwanja hiki bado ni kilekile miaka takaribani 40 iliyopita. Tarehe 21/3/2014 nilipita hapa. Kwa mbali naziona nyumba za walimu wa Sekondari Matombo.

Njia ya Msalaba ndani ya Kanisa Katoloki Matombo

Ijumaa ya tarehe  21 Machi 2014 nimebahatika kuhudhuria ibada ya njia ya msalaba kwenye kanisa langu la Matombo, Parokia ya Mt. Petri na Paulo. Tumsifu YESU KRISTU. AMINA.

Matombo Secondary School

Zamani ilijulikana kama Matombo Middle School. Sasa ni Matombo Secondary School. Shule hii ipo kijijini kwangu Kiswira, Matombo, Morogoro.Ilijengwa na wamisionari wakatoliki mwaka 1945. Shule hii imejengwa kwa ubora wa hali ya juu. Matombo ni moja ya shule zangu za msingi nilizowahi kusoma. Dirisha la nne kutoka kulia ni darasa mojawapo nililosoma mimi. Mwezi huu nimebahatika kurudi kijijini na kutembelea shule yangu.

Nyumba ya Martin Swangoni wa Kiswira Matombo

Nyumba hii ni moja ya nyumba za zamani kijijini Kiswira, Matombo, Morogoro. Nimesoma shule ya msingi nyuma ya nyumba hii ambapo sasa ni Matombo Sekondari. Nyumba hii nimeelezwa kuwa hapa zamani kulikuwa na duka kubwa! Hivi sasa imekarabatiwa lakini bati ni lilelile.

Kitu kiko Kiswira, Matombo

Kitu kimezungukwa na mazao mbalimbali-mapapai,migomba,minazi na michungwa. Hapa ni Matombo kijiji cha Kiswira, Morogoro

Saturday, March 22, 2014

Matombo maarufu kwa mazao ya tropiki

Hapa ni Matombo, kijijini Kiswira. Mazao ya aina mbalimbali ya kitropiki yanastawi kama inavyonekana pichani. Machungwa,migomba,minazi,muhogo,mashelisheli mananasi na maembe. Ugonjwa wa mnyauo unaoathiri migomba haujaingia sehemu hii. Kuna umuhimu wa kuweka mikakati ya uzalishaji wa zao la ndizi hapa Matombo kwa ajili ya chakula na kuongeza kipato cha wananchi wa sehemu hii  na kuimarisha pato la taifa. Watafiti wa Kilimo wanatakiwa kuongeza juhudi ya kutathmini sehemu hii na kuishauri serikali  jinsi ya kuwaendeleza wakulima wa eneo hili wakishirikiana na wagani.

Post yangu ya kwanza nikiwa Matombo

Jana tarehe 21/03/2014 niliwasili kijijini kwangu Matombo, Morogoro ni siku ya Ijumaa. Nilipata bahati kushiriki  Njia ya Msalaba ndani ya kanisa hilo nilimobatizwa, kupata Komunio ya Kwanza na Kipaimara. Waumini wachche waliohudhuria wengi walikuwa ni wanawake kuliko wanaume. Hali hii inafanana sana na Parokia yangu ya Vikindu Jimbo Kuu la Dar Es Salaam. Wanawake wengi wanatenga muda wao  kushiriki ibada  sisi wanaume tuko 'busy'. Namshukuru Mungu hii ni post yangu ya kwanza nikiwa Matombo baada ya miaka mingi sehemu hii ya Tanzania sasa imepata umeme tangu mwaka 2013 mambo haya sasa yanawezekana.

Thursday, March 20, 2014

Wanajua kula pilau

Si wote tunaofahamu kula pilau. Hawa ni wataalamu.

Limekuja kumbeba bi Harusi

    Limepambwa kwa khanga. Limekuja kumbeba bi harusi

Mwanamke nywele

   Kwenye Kitchen Party muonekano wa mwanamke ni kujiremba zikiwemo nywele!

Maandalizi ya chakula cha maulidi

Maandalizi chakula cha maulidi  wapishi ni akina baba kwanini?

Mzee Mbufu wa Utunge

   Mzee Mbufu akifuatilia kwa makini utaratibu wa kufunga ndoa wa kijana wake

Raha ya Maulid -Dufu

    Al-Kharat Islamic Centre-Mkuranga ikitoa burudani wakati wa Maulid 

Zawadi za Kitchen Party

Zawadi za Kitchen Party ya Mwajuma Pembe wa Kisemvule. Jamvi, ungo, mwavuli,ndoo,glassess,sahani,sufuria,vikombe.......... Mwanamke amekamilika

Najirusha

                     Raha ya rusha roho ni kujirusha